YANGA YAKUBALI KICHAPO CHA BAO 1-0 DHIDI YA BIASHARA

Yanga imeshindwa kutamba mbele ya Biashara United leo baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Karume


Bao pekee la Biashara United lilifungwa kwenye dakika ya 8 na Tariq Kiakal baada ya kuwazidi maarifa walinzi wa Yanga waliokuwa wakidhani ameotea
Ulikuwa ni mchezo uliotawaliwa na Biashara United kwa muda mwingi huku mazingira ya uwanja wa Karume yakitajwa kuwa kikwazo kikubwa kwa Yanga

Aidha mvua iliyonyesha wakati mchezo huo ukiendelea iiufanya uwanja uwe na mazingira magumu zaidi mpira kuchezeka kwa upande wa Yanga huku wenyeji wao wakionekana kuzoea hali hiyo
Baada ya mchezo huo Yanga inarejea jijini Dar es salaam kumalizia michezo mitatu iliyobaki

Aidha watani zao Simba nao wameendeleza uteja mbele ya Kagera Sugar baada ya kukabali kipigo cha bao 1-0 kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru