SIMBA YAENDELEZA UTEJA MBELE YA KAGERA SUGAR YAKUBALI KICHAPO CHA BAO 1-0

Kagera Sugar imeendeleza umwamba dhidi ya Simba baada ya leo tena kushinda kwa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru


Bao la kujifunga la beki Mohammed Hussein katika dakika ya 42 liliihakikishia Kagera Sugar alama tatu muhimu ambazo huenda zikawanusuru na janga la kuteremka daraja

Licha ya kosakosa kadhaa kutoka kwa Simba, mchezo huo ulimalizika kwa vijana wa Meckie Mexime kupata ushindi wa pili dhidi ya Simba msimu huu

Hata hivyo bado Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya Yanga nayo kuchezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Biashara United

Mchezo unaofuata ni dhidi ya Azam Fc, utapigwa May 13 katika uwanja wa Uhuru