Aussems ahakikishiwa mkataba mpya Simba

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems atasaini mkataba mwingine wa kuendelea kuifundisha timu hiyo baada ya mkataba wake wa awali kumalizika imefahamika

Aussems aliyetua Simba mwezi Julai mwaka jana, ametimiza masharti aliyopangiwa msimu uliopita ambapo alitakiwa kuifikisha timu hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa pamoja na kutwaa taji la ligi kuu

Chini yake Simba imefanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa na iko mbioni kukamilisha sharti la pili la kutwaa ubingwa wa ligi kuu

Inaelezwa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba chini ya Mwenyekiti wake Mohammed Dewji ‘Mo’ itampa Aussems mkataba wa mwaka mmoja na atasaini mkataba huo kabla ya kurejea kwao kwa ajili ya mapumziko baada ya ligi kumalizika