Ubingwa bado unaenda Simba, mechi tatu kuamua

Licha ya kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar jana, hesabu za kutwaa ubingwa kabla ya kucheza na Sevilla ziko palepale

Keshokutwa Jumatatu May 13 Simba itashuka uwanja wa Uhuru kucheza na Azam Fc katika mchezo ambao mabingwa hao watetezi wanahitaji ushindi

Katika mchezo wa duru ya kwanza Azam Fc ilipokea kichapo cha mabao 3-1

Baada ya mchezo huo Simba itacheza na Mtibwa Sugar May 16 kisha kucheza na Ndanda Fc May 19 michezo yote ikitarajiwa kupigwa uwanja wa Uhuru

Ushindi katika michezo hiyo mitatu utaifanya Simba ifikishe alama 90 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine

Aidha lengo la kukabidhiwa kombe kwenye mchezo dhidi ya Sevilla litafanikiwa kama Simba itashinda michezo hiyo iliyobaki

Simba imeshuka dimbani mara 32, inaongoza ligi ikiwa imejikusanyia alama 81 ikifuatiwa na Yanga yenye alama 80