Mabingwa wa kihistoria Yanga kesho Jumanne watashuka kwenye uwanja wa Uhuru kuikabili Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara hatua za lala salama
Baada ya kupoteza michezo miwili iliyopita dhidi ya Lipuli Fc (FA) na Biashara United, vijana wa Mwinyi Zahera wamepania kuondoka na alama zote tatu dhidi ya Ruvu Shooting
Kwenye mchezo wa kesho Yanga itamkosa beki wake Andrew Vicent mwenye kadi tatu za njano
Hata hivyo Yanga haina hofu ya kukosekana kwake kwani beki Abdallah Shaibu ‘Ninja’ yupo
Yanga imebakisha michezo mitatu ya kumaliza msimu na yote itapigwa kwenye uwanja wa Uhuru