Sare dhidi ya Azam Fc haikubadili mipango yetu – Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema licha ya timu yake kulazimishwa suluhu ya bila kufungana na Azam Fc, hakuna kilichobadilika juu ya mpango wa kutetea ubingwa

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya mchezo, Aussems alisema timu yake ilifanya jitihada zote za kusaka ushindi kwenye mchezo huo lakini walikosa bahati

Aidha amekosoa mbinu waliyotumia Azam FC kuwa hawakuwa na lengo la kushinda

“Tumejaribu kila mbinu kuweza kupata ushindi lakini imeshindikana. Sisi tulihitaji kushinda mchezo huu lakini mwenzetu walikuja kusaka alama moja na wameipata,” amesema

“Hata hivyo matokeo haya hayabadili chochote katika mipango yetu ya kutetea ubingwa”

Simba imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imefikisha alama 82

Bado hesabu za ubingwa ziko upande wao kwani wanahitaji alama nane tu ili kutawazwa mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Simba imebakisha michezo mitano