Mechi tano za kumaliza msimu Simba

Licha ya kutopata ushindi kwenye michezo miwili iliyopita, hesabu za ubingwa kwa Simba bado ziko salama ikihitaji kushinda angalau michezo mitatu kati ya mitano iliyobaki

Ratiba ya mechi zilizobaki za Wekundu hao wa Msimbazi inaonyesha keshokutwa May 16 watakuwa uwanja wa Uhuru kuikabli Mtibwa Sugar kisha kurejea tena uwanjani hapo May 19 kucheza na Ndanda Fc

May 21 Simba itasafiri kwenda mkoani Singida kuikabili Singida United kisha kurejea jijini Dar es salaam kucheza mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sevilla May 23

May 25 itarudi uwanja wa Uhuru kuikabili Biashara United na itamaliza msimu mkoani Morogoro kwa kuikabili Mtibwa Sugar May 28

Leave a comment