YANGA YAUTUMIA UWANJA WA UHURU VIZURI, YAICHAPA RUVU SHOOTING BAO 1-0

Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Ruvu Shooting bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru


Bao pekee la Yanga lilifungwa na Papi Tshishimbi aliyemalizia pasi murua ya Deus Kaseke kwenye dakika ya 16
Hilo lilikuwa bao la nne kwa Tshishimbi kwenye ligi msimu huu

Yanga ilikuwa bora kwenye kipindi cha kwanza na ilistahili kwenda mapumziko na angalau mabao mawili kama Raphael Daud asingekosa nafasi ya wazi
Ushindi huo umeifanya Yanga ifikishe alama 83 na kuiondoa Simba kileleni mwa msimamo wa ligi

Simba itacheza na Mtibwa Sugar keshokutwa Alhamisi katika mchezo ambao kama haitapata ushindi huenda ikafufua matumaini ya Yanga kwenye mbio za ubingwa

Leave a comment