Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba wameendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea taji lao baada ya leo kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru
Simba iliingia kwenye mchezo huo ikiwa na shauku ya kuondoka na alama zote tatu baada ya kutopata ushindi katika michezo miwili iliyopita
Ilianza kuhesabu bao la kwanza kupitia kwa nahodha John Bocco kwenye dakika ya 32 akiunganisha krosi murua iliyochongwa na Meddie Kagere
Simba iliyotawala mchezo huo, ilikwenda mapumziko ikiwa inaongoza kwa bao 1-0
cut
Kasi waliyomaliza nayo kipindi cha kwanza, waliiendeleza kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga mabao mengine mawili kupitia kwa Emmanuel Okwi(56′) na Clatous Chama (46′)
Mtibwa Sugar ilitumia zaidi mashambulizi ya kushitukiza na ilipoteza nafasi kadhaa kutokana na washambuliaji wake kutokuwa makini
Washambuliaji wa Simba wameendelea kuweka rekodi ya kuzifumania nyvu msimu huu, Simba ikifikisha mabao 72
Kagere, Bocco na Okwi wamefikisha mabao 50
Ushindi huo umeirejesha Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 85
Simba sasa inahitaji alama nne tu kutoka mechi nne zilizobaki ili iweze kutetea ubingwa