AISHI MANULA Aipania SEVILLA

Mlinda lango wa Simba Aishi Manula amesema mchezo dhidi ya Sevilla una maana kubwa kwa wachezaji wa timu hiyo kwani watakuwa na nafasi ya kuonyeshwa ukubwa wa timu yao

“Simba kucheza na Sevilla ndani ya uwanja wa Taifa ni jambo kubwa sana,” amesema

“Kwetu sisi wachezaji ni nafasi kubwa sana kuonyesha ubora wetu na kutimiza malengo ya timu yetu ambayo ni kufanya vizuri Kimataifa”

“Nawaalika mashabiki waje kwa wingi uwanja wa Taifa May 23 kuipa sapoti SImba, kuipa sapoti Tanzania”

Simba na Sevilla zitachuana Alhamisi, May 23 katika mchezo wa ‘kukata na shoka’ utakaopigwa uwanja wa Taifa kuanzia saa moja kamili jioni

Leave a comment