Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19

✍🏼 Mshambuliaji wa Klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu nchini Italia “Serie A” kwa msimu 2018/19, Cr7 ametwaa tuzo hii ikiwa ni msimu wake wa kwanza tu kusakata soka nchini Italia.
:
✍🏼 Ronaldo alikuwa sehemu ya kikosi cha Vibibi hivyo vya Turin kwenye kutwaa Scudetto yao ya nane mfululizo huku Cr7 ikiwa ni ya kwanza kwake na yeye mwenyewe akipachika Mabao yake 21 katika Ligi. Tuzo za Serie A kila mshindi anapewa baada ya kumalizika kwa msimu, lakini Ronaldo atapewa tuzo yake kabla ya mchezo wao dhidi ya Atalanta siku ya leo Jumapili.
:
✍🏼 Wachezaji wengine waliotwaa tuzo katika Ligi hiyo ni, Mlinda lango Bora wa Msimu katokea Inter Milan, Samir Handanovic, Beki Bora wa Msimu imebebwa na Muafrika kutoka Senegal, Kalidou Koulibaly anaekipiga Napoli, Kiungo Bora Ligi Kuu Italia imebebwa na fundi wa kumiliki Dimba La Kati, Sergej Milinkovic-Savic kutoka Klabu ya Lazio, Fabio Quagliarella Mshambuliaji hatari wa Sampdoria kabeba tuzo ya Mshambuliaji bora wa msimu na Nicolo Zaniola kinda ambaye anacheza Klabu ya AS Roma, yeye kaibuka Mchezaji bora kijana wa Mwaka ndani ya Serie A.
:
✍🏼 Ronaldo Sasa katwaa tuzo ya Mchezaji bora wa mwaka Italia, England na Hispania pamoja na kutwaa Ubingwa wa Ligi kwa nchi zote tatu.. Koulibaly amekuwa nguzo ya ulinzi ndani ya Napoli blocks 31, Clearance 125, tackles won 60 Kati ya 67, clean sheets 13 katika mechi 31 alizocheza..
#seriea #juventus #napoli #lazio #asroma
@Sokawaytz

Leave a comment