NOEL MWANDILA OUT YANGA -Mwenyikiti wa klabu ya Yanga, Dr Mbette Mshindo Msolla amethibitisha kuwa wataachana na kocha msaidizi wa klabu hiyo Noel Mwandila na kuajiri kocha msaidizi mzawa ili aweze kumsaidia kocha Mwinyi Zahera. -Akiongea kuhusu kuibadili Yanga amedai wafanyakazi wote wa Yanga na watu wa bechi la ufundi isipokuwa kocha mkuu Mwinyi Zahera wanatakiwa kutuma CV zao upya kwa uongozi mpya ili kufanyiwa kazi na kila mtu afanye kazi anayostahili. -Kuhusu kocha Msaidizi Mwenyekiti alisema “Benchi la ufundi linahitaji kuwa na kocha msaidizi mwenye kiwango kizuri ili kuongeza nguvu ndani ya kikosi chetu, tutaangalia zaidi kocha mzawa ili aweze kuwa sambamba na kocha Zahera kufanya kazi.” “Katika nchi za wenzetu zilizoendelea kocha mkuu amekuwa akimtumia zaidi kocha msaidizi kwa kumtuma kwa ajili ya kwenda kufuatilia wachezaji wanaowahitaji kwa ajili ya kuwasajili hata ikiwa nje ya nchi ambaye anafuatilia mechi na mazoezi anayofanya mchezaji, hivyo tunahitaji msaidizi mwenye weredi atakayeshirikiana vyema na kocha mambo mbalimbali” “Tukiachana na kazi ya kutafuta kocha, pia tutawatumia wachezaji wa zamani waliowahi kuichezea Yanga kuweza kuwatuma mikoani kwa ajili ya kusaka vipaji,”
Alisema Dr. Mshindo Msolla -Noel Mwandila alijunga na klabu ya Yanga misimu miwili iliyopita kama kocha wa viungo chini ya kocha George Lwandamina ila baada ya kuondoka kwa Lwandamina na Shadrack Nsajingwa ndio akawa kocha msaidizi wa klabu ya Yanga.
.
Cc : Yossima Sitta Jr