Yanga imeendeleza umwamba wake katika dimba la Uhuru baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara mzunguuko wa 37
Bao pekee la Yanga lilipatikana kwenye dakika ya 26 likiwekwa kimiani na Heritier Makambo aliyeunganisha kwa kichwa krosi ya Haji Mwinyi
Hilo ni bao la 17 kwa Makambo, akishika nafasi ya pili sawa na Salim Aiyee katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu nyuma ya Meddie Kagere wa Simba mwenye mabao 23
Licha ya kuwakosa nyota wake wengi ambao ni wagonjwa na majeruhi, Yanga ilitandaza kandanda safi na kutawala mchezo huo kwa muda mwingi
Kiungo kinda Gustapha Simon ameendelea kudhihirisha ubora wake, hakuna shaka msimu ujao atapata nafasi zaidi kwenye kikosi cha Zahera
Yanga imefikisha alama 86 sasa ikibakiwa na mchezo mmoja wa kumaliza msimu dhidi ya Azam Fc
Mchezo huo utapigwa May 28 2019