IBRAHIM AJIBU AMALIZANA NA TP MAZEMBE.

Nahodha wa Klabu ya Yanga SC, Ibrahim Ajib anatarajia kujiunga na Mabingwa wa DR Congo, Miamba wa Lubumbashi Klabu ya TP Mazembe kwa uhamisho huru Baada ya Mkataba wake na Klabu yake ya Jangwani kufikia tamati mwishoni mwa mwezi Ujao.. 👏👏👏.
#transfers
.

Klabu ya TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuwaeleza kuwa wamefanya makubaliano ya kuingia mkataba na Ibrahim Ajibu utakaoanza rasmi Julai 1.

Hiyo ni baada ya Mazembe kujiridhisha kuwa mkataba wa mchezaji huyo na Yanga unaisha Juni 30.

Taarifa hii inaua matumaini ya Wanajangwani hao kuendelea kuwa na fundi huyo wa mpira msimu ujao huku ikizima tetesi za kurejea Simba.

#TransferUpdates

Leave a comment