Mabingwa wa nchi Simba leo wanakabidhiwa taji la pili mfululizo ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya mchezo dhidi ya Biashara United
Mchezo huo utaanza mapema tu, saa tisa Alasiri ambapo hafla ya makabidhiano ya ubingwa itafanyika baada ya mchezo huo
Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Kangi Lugola anatarajiwa kuwa mgeni wa rasmi katika hafla hiyo itakayofanyika uwanja wa Taifa
Uongozi wa Simba umewataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa leo kushuhudia tukio hilo litakalobaki kwenye kumbukumbu za klabu ya Simba
Hilo ni taji la 20 la ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Simba
Baada ya kuichachafya Sevilla juzi, Aussems amepania kushusha mziki kamili ili kunogesha sherehe za ubingwa kwa ushindi mnono
Viingilio vya mchezo huo, VIP A Tsh 15,000/- VIP B na C Tsh 10,000/- wakati mzunguuko ni Tsh 3,000/-