KAMUSOKO -:Aaga wachezajinyanga

Kiungo mkongwe Thabani Kamusoko yuko Zimbabwe na kikosi cha timu ya Taifa kinachojiandaa na fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika mwezi ujao nchini Misri

Ni kama kiungo huyo hatarejea tena Yanga baada ya jana kuwaaga wachezaji wenzake wa kikosi cha Yanga

“Nimewakumbuka sana rafiki zangu, sina neno jingine la kusema zaidi kwani mlikua zaidi ya marafiki,” ameandika Kamusoko ukurasa wake wa Instagram

Kamusoko ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu, hatma yake ikibaki mikononi mwa kocha Mwinyi Zahera

Keshokutwa Jumanne baada ya mchezo dhidi ya Azam Fc, Yanga itatangaza majina ya wachezaji ambao wameachwa pamoja na wale ambao tayari wamesajiliwa na timu hiyo

Zahera amesema kuna wachezaji nane ambayo tayari wamesajiliwa na timu hiyo, sita wa Kimataifa na wawili wazawa