Aliyekuwa kiungo wa Azam FC Tafadzwa Kutinyu ambaye alikuwa akihusishwa na Yanga, amesajiliwa na klabu ya Horoya AC, mabingwa wa Guinea
Kutinyu ametua timu hiyo akiwa mchezaji huru baada ya mkataba wake na Azam Fc kumalizika
Kutinyu anaungana na Heritier Makambo ambaye anasubiri kujiunga na timu hiyo baada ya ligi kumalizika
Kutinyu yuko kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Zimbabwe kinachojiandaa na fainali za AFCON 2019 zitakazofanyika Misri
Kutinyu na Thabani Kamusoko ni wachezaji pekee kutoka Tanzania walioitwa timu ya Taifa ya Zimbabwe