– Kiungo wa timu ya Taifa ya England, Dele Alli amesaini mkataba mpya wa miaka Sita (6) Kuendelea kuichezea Klabu yake ya Tottenham Mpaka mwaka 2024..
.
– Dele Alli Alijiunga na Spurs mwaka 2015 akitokea MK Dons, na tokea hapo akawa ni Mmoja wa Wachezaji bora Barani Ulaya chini ya kocha wake Mauricio Pochettino.
.
– Tokea ajiunge na Klabu hiyo ya London amefanikiwa kufunga Magoli 48 na Assist 41 Katika mechi 153 akiwatumikia farasi weupe.
.
– Tottenham wanawaongeza Mikataba mipya Wachezaji wao Wote Ambao ni tegemeo, kabla ya Alli walitoka kumpa Mkataba mpya Mshambuliaji wao Hary Kane ambaye alisaini mwezi juni mkataba unaofikia kikomo mwaka 2024 pia Spurs walimuongeza mkataba wa miaka mitano kocha wao mkuu Mauricio Pochettino..
.
– Spurs Sasa wanahakikisha wanawafunga Wachezaji wao muhimu Kwa Mikataba ya muda mrefu kabla ya kufikia mwaka 2019 na ndio mwaka Ambao wataamia rasmi Katika Uwanja wao wa White Hart Lane uliokuwa Katika ukarabati wa Kuongeza ukubwa ambapo kwasasa wanatumia Uwanja wa Taifa “Wembley Stadium”