ADAM SALAMBA: Aahidi kuendeleza motto wa mabao simba Sc

Mshambuliaji Adam Salamba, amesema kitendo cha kufunga kwenye michezo miwili iliyopita kimemuongezea hamu ya kuendelea kufanya vizuri zaidi msimu huu.

Salamba amesema ameongeza kujiamini na sasa anataka kutumia vema kila nafasi atakayopewa na kocha wake kuitumikia timu hiyo.

“Nafurahi kwa sababu napata nafasi ya kucheza na nimeanza kuonyesha kile ambacho Wanasimba wanakitaka kutoka kwangu…, ingawa muhimu ni ushindi kwa timu lakini pia ninapopata nafasi ya kufunga kwangu ni furaha zaidi,” alisema Salamba.

Salamba ambaye alijiunga na Simba msimu huu akitokea Lipuli ya Iringa, amefunga mara mbili mfululizo kwenye michezo iliyopita dhidi ya Alliance ya Mwanza na Ruvu Shooting.

Katika michezo hiyo, Simba ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-1 (dhidi ya Alliance) na baadaye 5-0 (dhidi ya Ruvu Shooting).

Kikosi hicho cha kocha Patrick Aussems, kitashuka tena dimbani wiki hii kuumana na JKT Tanzania ambao wameamishia mechi hiyo kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Simba imefikisha pointi 23 baada ya kucheza michezo 10 ikiwa nafasi ya tatu nyuma ya Yanga na Azam fc