MLIPILI: Atoweka Kikosini Simba sc

Inaelezwa beki chipukizi wa Simba Yusufu Mlipili ameondoka kikosini na viongozi wa timu hiyo hawajui alipo.

Mlipili aliyekuwa mmoja wa wachezaji wa kutegemewa kwenye kikosi cha Simba msimu uliopita, amekumbana na wakati mgumu wa kupata namba msimu huu.

Inaelezwa beki huyo aliyesajiliwa kutoka klabu ya Toto Africans hajaonekana kwenye mazoezi ya Simba kwa takribani wiki moja sasa.

“Hatujui alipo, kwa sababu hatuna taarifa rasmi juu ya kukosekana kwake,” kimesema chanzo

Usajili wa Paschal Wawa na kurejea kwa Juuko Murshidi kumemuweka kwenye wakati mgumu beki hiyo ambaye alitabiriwa kuwa na mafanikio makubwa siku za baadae