Simba Sc Kuivaa JKT Tanzania

Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba Jumamosi ijayo Novemba 03 kitakuwa mkoani Tanga kupepetana na maafande wa JKT Tanzania kwenye mchezo wa ligi kuu.

Awali TFF ilitangaza kufuta michezo ya Simba, Yanga na Azam iliyokuwa ipigwe wiki ya kwanza ya mwezi Novemba ili kutoa nafasi kwa wachezaji wa timu hizo walio kwenye kikosi cha Stars kujuishwa kambini nchini Afrika Kusini.

Hata hivyo michezo hiyo itapigwa kama kawaida.

Hivi karibuni TFF iliiruhusu JKT Tanzania kutumia uwanja wa Mkwakwani kwa ajili ya michezo yake dhidi ya Simba na Yanga.