SIMBA 2- JKT TANZANIA

Mabingwa watetezi ligi kuu ya Tanzania Bara Simba leo wametakata uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga baada ya kuilaza JKT Tanzania mabao 2-0.

Alikuwa ni mshambuliaji hatari Meddie Kagere ‘MK14’ aliyepeleka kilio kwa maafande wa JKT baada ya kuifungia Simba mabao yote mawili.

Alifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 12 kwa shuti kali akiwa ndani ya 18 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Emmanuel Okwi.

Mpira wa adhabu uliopigwa na Okwi kwenye dakika ya 38 uligonga mwamba kabla ya kukutana na guu la Kagere kwa mara nyingine na kuiandikia Simba bao la pili.

Licha ya changamoto ya uwanja, kikosi cha Simba kilicheza kandanda safi muhimu zaidi ikiwa ni kufanikiwa kuondoka na alama zote tatu dhidi ya JKT Tanzania, moja ya timu ngumu kabisa kwenye ligi msimu huu.

Ushindi huo umeirejesha Simba kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 26.

Kagere amefikisha mabao saba sawa na Okwi wote wakiwa nyuma ya Eliudi Ambokile wa Mbeya City aliyefunga mabao nane.

Matokeo ya michezo ya leo

Leave a comment