Michuano Ya Sportpesa kufanyika January 2019

Michuano ya SportPesa Super Cup inayodhaminiwa na Kampuni ya SportPesa inatarajiwa kufanyika nchini Tanzania kuanzia January 22 hadi January 27 2019.

Michezo hiyo inatarajiwa kupigwa dimba la Uhuru na CCM Kirumba.

Akizungumza na waandishi wa Habari kwenye Ukumbi wa Hostel za Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF), Mkurugenzi mtendaji wa SportPesa Tarimba Abas amesema timu nane zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo.

Timu hizo ni Simba, Yanga, Singida United FC na Mbao FC zote kutoka Tanzania huku upande wa Kenya ni Gor Mahia, AFC Leopards, Bandari na Kariobangi Sharks.

Tarimba amesema Mbao Fc imealikwa kwenye michuano hiyo ya tatu kutokana na Klabu hiyo kuonyesha ushindani mkali katika Ligi kuu ya Tanzania Bara.

Bingwa wa michuano hiyo atajinyakulia kitita cha dola 30,000 pamoja na kukata tiketi ya kwenda nchini Uingereza kucheza na Everton Fc

Leave a comment