TFF ilivyokosa Msimamo kwa nafasi ya MANJI yanga Sc

Julai 11 2018 Shirikisho la soka nchini (TFF) lilimuondoa kwenye nafasi yake aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Clement Sanga baada ya kupokea barua kutoka kwa uongozi wa Yanga ikimtambulisha Yusufu Manji kuwa amerejea klabuni hapo.

Sanga aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Yanga alipoteza sifa ya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi baada ya TFF kuikubali barua ya Yanga iliyomtambulisha Manji kuwa Mwenyekiti baada ya kuridhia kurejea.

Sifa ya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu ni lazima uwe Mwenyekiti wa timu inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara.

Hata hivyo uamuzi huo uliotolewa miezi minne iliyopita na TFF ni kinyume kabisa na uamuzi wao wa sasa wa kuitaka Yanga ifanye uchaguzi wa kujaza nafasi ya Manji licha ya kuwa tayari walishamtambua na uamuzi wao huo ulisababisha Sanga akapoteza kibarua chake kwenye Bodi ya Ligi.

Inafahamika uamuzi wa sasa umetolewa na BMT na TFF ni watekelezaji tu lakini ni wazi TFF imeonyesha kutokuwa na msimamo katika jambo hili la uchaguzi wa Yanga hasa kwenye nafasi ya Mwenyekiti

Leave a comment