USAJILI: Simba kumsajili mchezaji huyu?

Mapema leo katika ukurasa rasmi wa klabu ya Simba mtandao wa Instagram iliwekwa picha ya beki kutoka klabu ya Asec Mimosas, Zana Oumar Coulibaly

Coulibaly ni mlinzi wa kulia anayetarajiwa kusajili na Simba kuziba pengo la Shomari Kapombe

Hiyo ni habari njema kwa mashabiki wa Simba kwani Coulibaly huenda akawa njiani kutua Msimbazi.

Ingawa picha hiyo haikuwa na maelezo mengi, ni dhahiri uongozi wa Simba utakuwa umemalizana na mkali huyo.