USAJILI: Simba yamsajili beki huyu

Simba imemnasa beki wa kulia wa klabu ya Asec Mimosas Zana Coulibaly.

Mchezaji huyo atawasili nchini leo kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usajili.

Beki huyo anatarajiwa kuziba pengo la Shomari Kapombe ambaye atakuwa nje kwa muda mrefu baada ya kupata majeraha wakati akiitumikia timu ya Taifa

“Tunapenda kuwatangazia kwamba beki Zana Coulibaly kutoka ASEC Mimosas ya Ivory Coast leo atawasili nchini kwa ajili kukamilisha taratibu za mwisho kujiunga na timu yetu ili kuziba pengo la beki Shomari Kapombe ambaye siku za karibuni alipata majeraha,” imesema taarifa ya Simba