Mlinzi wa pembeni kutoka klabu ya Asec Mimosas Zana Coulibaly leo amefanyiwa vipimo vya afya Hospitali ya Muhimbili tayari kusaini mkataba wa kuitumikia Simba
Zana aliyetua jana, inaelezwa amefuzu vipimo hivyo na anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba
Beki huyo mwenye ‘mapafu ya mbwa’ amesajiliwa ili kuziba pengo la Shomari Kapombe aliyeumia mwezi uliopita wakati akiitumikia timu ya Taifa
Kapombe anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini.
Zana anatarajiwa kutumika kwenye ligi tu kwa kuwa atakuwa amechelewa usajili wa CAF.
Hata hivyo mchezaji huyo ataweza kuongezwa kwenye kikosi cha Simba kinachoshiriki michuano hiyo kama mabingwa hao wa Tanzania Bara watafuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo ya CAF
