Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa kulia Zana Coulibaly kutoka klabu ya Asec Mimosas ya ivory Coast.
Coulibaly aliyefuzu vipimo vya afya jana amesaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia mabingwa hao wa Tanzania Bara.
Coulibaly raia wa Burkina Faso amesajiliwa rasmi leo Ijumaa mchana na alikabidhiwa uzi wa Simba na kocha Mkuu Patrick Aussems mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Simba Cresentius Magori