Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba leo kimeendelea na mazoezi nchini Zambia kujiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Nkana Fc utakaopigwa Jumamosi.
Mabingwa hao wa kihistoria wa soka Afrika Mashariki wameendelea kujifua katika uwanja wa Dynamos walioanza kuutumia jana.
Kesho Simba inatarajiwa kujifua kwenye uwanja wa Nkana utakaotumika katika mchezo wa keshokutwa.




