
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems leo alipanga kikosi cha maangamizi ambacho kwa hakika kimeingamiza Singida United iliyokuwa na wakati mgumu katika mchezo huo.
Shiza Kichuya leo alikuwa nyota wa kikosi cha Simba baada ya kuhusika katika mabao yote yaliyofungwa na washiriki hao wa michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi
Katika dakika ya 17 Kichuya alimtengenezea Bocco aliyefunga bao lake la tatu msimu huu huku Kichuya tena akifunga mabao mengine mawili kwenye kipindi cha pili yote yakitengenezwa na Cletous Chama ‘CCC’

Ushindi ni matokeo stahiki kwa Simba iliyochocheza kandanda safi kwa muda wote wa mchezo.
Simba imefikisha alama 33 baada ya ushindi wa leo, imeendelea kusalia katika nafasi ya tatu.
Kama itashinda michezo yake minne ya kiporo, Simba ina uhakika wa kuiengua Azam Fc katika nafasi ya pili.
Leo Azam imepoteza mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar kwa kuchapwa mabao 2-0