
Katika mchezo huo, licha ya kutawala kwa muda mwingi, Simba ililazimika kusubiri hadi dakika ya 84 kupata bao pekee la ushindi lililofungwa na Rashid Juma.
Ushindi huo umeifanya Simba ifikishe alama sita na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo.
Nyoni aumia
Aidha, kwenye mchezo huo Simba ilipata pigo baada ya beki wake kiraka Erasto Nyoni kupata majeraha ya goti mwishoni mwa kipindi cha kwanza.
Uongozi wa Simba unatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu majeraha ya mchezaji huyo tegemeo wa kikosi cha kwanza ambacho Jumamosi ijayo kinakabiliwa na mchezo wa ligi ya mabingwa hatua ya makundi dhidi ya JS Sauora