FT : Azam Fc 2-1 Simba

Azam Fc wamefanikiwa kutwaa taji la kombe la Mapinduzi kwa msimu wa tatu mfululizo baada ya kuichapa Simba mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliopigwa leo kisiwani Pemba.

Azam Fc ilionekana kuwa imara zaidi na ilitangulia kufunga bao la kuongoza kupitia kwa Mdathir Yahya kwenye dakika ya 44 kabla beki Yusufu Mlipili haijairudisha Simba mchezoni kwenye dakika ya 62

Obrey Chirwa ndiye aliyeifungia Azam Fc bao la ushindi kwenye dakika ya 72.

Azam Fc walidhamiria kufanya vizuri katika michuano hiyo wakati Simba imeathiriwa kwa kiasi kikubwa na ushiriki wake wa michuano ya ligi ya mabingwa kwani haikuwa na wachezaji wake wa kikosi cha kwanza ambao jana waliichapa JS Saoura mabao 3-0