FT : Simba 2-1 AFC Leopards

Simba imetinga nusu fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup baada ya kuilaza AFC Leopards mabao 2-1 katika mchezo wa robo fainali uliopigwa uwanja wa Taifa leo

Mabao ya Simba yalipatikana katika kila kipindi yakifungwa na Emmanuel Okwi na Clatous Chama

Okwi aliifungia Simba bao la kuongoza kwenye dakika ya 13 akimalizia kwa ufundi kabisa krosi ya Zana Coulibaly

Licha ya AFC Leopards kumiliki mpira kwa muda mwingi lakini ni Simba iliyokuwa hatari zaidi kila ilipokuwa na mpira kwa kupeleka mashambulizi ya kasi langoni kwa Leopards

Okwi aliyekuwa mwiba mkali kwa safu ya ulinzi ya Leopards alisababisha bao la pili lililofungwa na Chama aliyemalizia krosi murua iliyomiminwa na mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Uganda

Leopards ilipata bao la kufutia machozi kwenye dakika ya 61 kupotia kwa Oburo

Katika mchezo huo kocha Patrick Aussems aliwapa nafasi Lamine Moro na mshambuliaji Hunlede Kisimbo walio kwenye majaribio ya kusajiliwa na mabingwa hao wa Tanzania Bara

Baada ya ushindi huo Simba imeungana na Mbao Fc, K. Sharks na Bandari kutinga hatua ya nusu fainali

Michezo ya nusu fainali itapigwa Ijumaa, Januari 25 2019