
Simba ilitangulia kupata bao la kuongoza kwenye dakika ya 45 mfungaji akiwa Meddie Kagere aliyeachia shuti kali akiwa ndani na 18
Hata hivyo Bandari Fc ilirejea mchezoni kwenye kipindi cha pili ikisawazisha kupitia mkwaju wa penati kwenye dakika ya 59 baada ya Mzamiru Yassin kumfanyia madhambi Abdallah Khamis ndani ya eneo la hatari
Mzamiru alilazimika kukimbizwa Hospitalini kwa matibabu zaidi baada ya kuumia kwenye tukio hilo
Bandari Fc ilifunga bao la pili kwenye dakika ya 72 kupitia kwa Lugogo
Simba haikuwa kwenye kiwango bora leo, pengine muda wa saa nane uliopigwa mchezo huo haukuwa rafiki kwa wachezaji kutokana na joto la jijini Dar es salaam
Hata hivyo hiyo haiwezi kutumika kama sababu ya kufungwa kwa kuwa hata Bandari Fc ilicheza katika mzingira hayo hayo
Simba sasa itacheza kusaka nafasi ya tatu ikitarajiwa kuchuana na timu itakayopoteza kwenye mchezo wa pili wa nusu fainali kati ya Mbao Fc dhidi ya K Sharks