FT : Simba yaitunga Mbao Fc 5-3 kwa matuta baada ya sare

Simba imefanikiwa kumaliza nafasi ya tatu kwenye michuano ya SportPesa Cup baada ya kupata ushindi wa penati 5-3 kufuatia matokeo ya 0-0 dhidi ya Mbao Fc katika mchezo uliopigwa uwanja Taifa

Simba iliutawala mchezo huo kwa muda mwingi ikikosa nafasi kadhaa huku mlinda lango wa Mbao Fc Metacha Mnata akiibuka nyota wa mchezo baada ya kuikoa timu yake na kipigo

Aidha, Haikuwa siku nzuri kwa mshambuliaji Sadney Urikhob aliye kwenye majaribio katika kikosi cha Simba kwani alikosa nafasi kadhaa za kufunga leo
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wachezaji wake walicheza vizuri leo lakini walishindwa kufunga kutokana na kukosa umakini kwa washambuliaji wake huku akimsifia mlinda lango wa Mbao Fc Metacha kwa kuzuia michomo mingi iliyoelekezwa langoni kwake
Simba imejinyakulia kitita cha dola 7,500 baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu huku Mbao Fc ikipata dola 5,000