
Simba iliutawala mchezo huo kwa muda mwingi ikikosa nafasi kadhaa huku mlinda lango wa Mbao Fc Metacha Mnata akiibuka nyota wa mchezo baada ya kuikoa timu yake na kipigo
Aidha, Haikuwa siku nzuri kwa mshambuliaji Sadney Urikhob aliye kwenye majaribio katika kikosi cha Simba kwani alikosa nafasi kadhaa za kufunga leo
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema wachezaji wake walicheza vizuri leo lakini walishindwa kufunga kutokana na kukosa umakini kwa washambuliaji wake huku akimsifia mlinda lango wa Mbao Fc Metacha kwa kuzuia michomo mingi iliyoelekezwa langoni kwake
Simba imejinyakulia kitita cha dola 7,500 baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu huku Mbao Fc ikipata dola 5,000