
Baada ya Lipuli Fc kunusurika katika michezo mitatu iliyopita, leo Simba imepata matokeo stahili baada ya kuwabana vilivyo vijana hao wa Selemani Matola ambaye kabla ya mchezo alitamba kuwa hataki sare
Clatous Chama aliitanguliza Simba mapema tu kwenye dakika ya tano kwa kufunga bao safi kabla Lipuli Fc hawajasawazisha kupitia kwa Paul Nonga kwenye dakika ya 18
Chama tena akaongeza la pili dakika chache kabla ya kwenda mapumziko na Meddie Kagere aliye katika kiwango bora kabisa cha kupachika mabao , akafunga bao la tatu kwenye dakika ya 58
Ushindi huo umeendelea kuisogeza Simba kileleni baada ya kufikisha alama 48, sasa ikiwa nyuma ya Azam Fc kwa tofauti ya alama mbili
Kituo kinachofuata ni Shinyanga ambapo Jumapili, March 03 Simba itachuana na Stand United katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Kambarage