FT : Al Ahly 5-0 Simba

Simba imepoteza mchezo wa pili wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya kukubali kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Al Ahly katika mchezo wa mzunguuko wa tatu, kundi D

Al Ahly ilitumia dakika 40 kufunga mabao yake yote matano wakitumia makosa ya safu ya ulinzi ya Simba iliyokuwa ikijichanganya mara kwa mara

Ni mchezo ambao kiufundi ulimalizika katika kipindi cha kwanza baada ya Al Ahly kufunga mabao hayo matano

Simba imeruhusu mabao 10 katika michezo miwili ya ligi ya mabingwa iliyopita

Kocha Patrick Aussems huenda akahitaji kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza hasa kwenye safu ya ulinzi ili kuweza kufanya vizuri katika michezo miwili ya nyumbani iliyobaki

Mchezo unaofuata utapigwa wiki ijayo katika dimba la Taifa dhidi ya Al Ahly

Licha ya kipigo hicho Simba imeendelea kusalia nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi D ikiwa na alama tatu

Al Ahly imejikita kileleni mwa kundi hilo baada ya kufikisha alama saba

Vita Club inashika nafasi ya pili ikiwa na alama nne baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 nyumbani dhidi ya JS Saoura katika mchezo mwingine wa kundi ambao ulipigwa mapema

JS Saoura inashika nafasi ya nne ikiwa na alama mbili