
Ulikuwa ni mchezo ambao mzani ulielemea upande wa Simba hata kabla mchezo huo haujapigwa kutokana na ubora wa kikosi cha Simba

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika kwa timu hizo kutofungana licha ya Simba kutawala kwa muda mwingi
Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Patrick Aussems kwa kumtoa Chama na kumuingiza Dilunga kwenye kipindi cha pili yaliongeza umakini kwa wekundu wa Msimbazi na Dilunga ndiye aliyesaidia kupatikana kwa bao la Simba
Bao hilo pekee lilifungwa na Meddie Kagere katika dakika ya 72 akimalizia pasi murua ya nahodha John Bocco
Hilo lilikuwa bao la tisa kwa Kagere kwenye ligi msimu huu
Ushindi huo umeiweka Simba katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wake dhidi ya wapinzani wao Yanga
Imefikisha alama 39 na kuchupa mpaka nafasi ya tatu.
Kama Simba itashinda michezo yake yote ya viporo itakuwa na uhakika wa kuwazidi alama tano wapinzani wao Yanga.