Ajib mgonjwa, kuikosa Lipuli Fc

Nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib ameondolewa katika kikosi kinachosafiri kwenda mkoani Iringa baada ya kuugua

Yanga itaikabili Lipuli Fc bila ya kuwa na mpishi wake huyo wa mabao aliyehusika katika mabao 21 kati ya 45 yaliyofungwa kwenye ligi

Hata hivyo kukosekana kwake hakuwezi kuwa tatizo kwa kikosi cha Mwinyi Zahera kilichosheheni viungo wengi

Mohammed Issa ‘Banka’, Thabani Kamusoko na Haruna Moshi ‘Boban’ wote wanaweza kucheza nafasi yake.

Kwa michezo ya hivi karibuni, Ajib amekuwa akitokea benchi kuongeza nguvu kwenye kipindi cha pili

Changamoto pekee inayoikabili Yanga huenda ikabaki kwenye safu ya ulinzi baada ya kukosekana kwa Andrew Vicent ambaye ni majeruhi na Abdallah Shaibu ‘Ninja’ aliyefungiwa michezo mitatu

Kocha Noel Mwandila huenda akalazimika kumtumia kiraka Said Juma Makapu kwenye nafasi ya ulinzi sambamba na mkongwe Kelvin Yondani.

Pia yupo beki aliyepandishwa kutoka Yanga B Cleosaf Sospeter