Djuma aitakia kheri Simba

Kocha Mkuu wa AS Kigali inayoshiriki ligi kuu ya Rwanda, Masudi Djuma ameitakia kheri Simba ili iweze kushinda mchezo dhidi ya AS Vita Club na kuweza kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Djuma aliyewahi kuhudumu Simba akiwa kocha msaidizi kwa misimu miwili, amesema Simba itakayokuwa nyumbani ina kila sababu ya kushinda mchezo huo Jumamosi

“Timu zinazoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu zimetumia vyema viwanja vyao vya nyumbani. Naamini Simba itatumia uwanja wake vizuri pia,” Djuma aliiambia Radio eFM

Djuma aliondolewa Simba mwezi Oktoba mwaka jana baada ya kutofautiana na kocha Mkuu Patrick Aussems.

Nafasi yake tayari imechukuliwa na kocha Denis Kitambi

Djuma anabaki kuwa miongoni mwa makocha waliopita Simba na kukubalika sana na mashabiki wa timu hiyo