
Inaelezwa Ajib ambaye mkataba wake na Yanga unamalizika mwishoni mwa msimu, tayari amesaini mkataba wa awali kurudi Msimbazi
Ajib alisajiliwa na Yanga mwaka juzi akipishana na Haruna Niyonzima aliyetua Msimbazi
Simba tayari imeanza mkakati wa kukiboresha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao ambapo mbali na Ajib, mabingwa hao wa Tanzania Bara inaelezwa tayari wametua nchini Kenya kumnyakua mshambuliaji wa Gor Mahia, Jacques Tuyisenge

Tuyisenge aliyeisaidia Gor Mahia kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho Barani Afrika, ataondoka Gor Mahia mwishoni mwa msimu mkataba wake utakapokuwa umemalizika
Msimu uliopita Tuyisenge alikuwa pacha wa Meddie Kagere katika kikosi cha Gor Mahia kilichokuwa kikinolewa na Dylan Kerr