Ajib, Tuyisenge watajwa Msimbazi

Nahodha wa Yanga Ibrahim Ajib huenda akarejea katika klabu ya Simba, mahali alipokuza jina lake kwenye soka

Inaelezwa Ajib ambaye mkataba wake na Yanga unamalizika mwishoni mwa msimu, tayari amesaini mkataba wa awali kurudi Msimbazi

Ajib alisajiliwa na Yanga mwaka juzi akipishana na Haruna Niyonzima aliyetua Msimbazi

Simba tayari imeanza mkakati wa kukiboresha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao ambapo mbali na Ajib, mabingwa hao wa Tanzania Bara inaelezwa tayari wametua nchini Kenya kumnyakua mshambuliaji wa Gor Mahia, Jacques Tuyisenge

Tuyisenge aliyeisaidia Gor Mahia kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho Barani Afrika, ataondoka Gor Mahia mwishoni mwa msimu mkataba wake utakapokuwa umemalizika

Msimu uliopita Tuyisenge alikuwa pacha wa Meddie Kagere katika kikosi cha Gor Mahia kilichokuwa kikinolewa na Dylan Kerr