Yanga yajifua Mwanza tayari kuikabili Alliance Fc

Kikosi cha Yanga jana jioni kilifanya mazoezi kwenye uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba kujiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA (ASFC) dhidi ya Alliance Fc

Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa CCM Kirumba

Vinara hao wa ligi kuu ya Tanzania Bara walitua jana asubuhi jijini Mwanza wakiongozwa na kocha Mwinyi Zahera

Jioni ya leo Ijumaa Yanga inatarajiwa kufanya mazoezi yake ya mwisho kwenye dimba la CCM Kirumba tayari kwa mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa jiji la Mwanza na maeneo ya jirani