
Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa CCM Kirumba
Vinara hao wa ligi kuu ya Tanzania Bara walitua jana asubuhi jijini Mwanza wakiongozwa na kocha Mwinyi Zahera
Jioni ya leo Ijumaa Yanga inatarajiwa kufanya mazoezi yake ya mwisho kwenye dimba la CCM Kirumba tayari kwa mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa jiji la Mwanza na maeneo ya jirani