
Jumamosi, Simba ililazimishwa suluhu ya ila kufungana dhidi ya TP Mazembe, kwenye mchezo wao wa robo fainali uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar res Salaam.
Matokeo hayo yanailazimu Simba kupata ushindi au sare yoyote ya mabao ugenini ili iweze kutinga nusu fainali
Mchezo wa marudiano utapigwa Aprili 13, nchini Congo kwenye Uwanja wa TP Mazembe.
Kagere alisema anaamini kwa juhudi walizonazo, bado wana nafasi ya kushinda mchezo wao huo.
Alisema kiwango chao si kibaya na hata juzi walicheza vizuri, wakienda ugenini hata kama watatoka sare haitakuwa mbaya.
“Mazembe ni timu kubwa na tulicheza vizuri ila tulikosa bahati ya kupata mabao, tayari tunawajua vizuri hivyo tutacheza zaidi ya tulivyopambana nyumbani, mashabiki wasikate tamaa,” Kagere amenukuliwa na Bingwa
Simba inatarajiwa kuondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya Alhamisi kuelekea nchini Congo tayari kwa mchezo huo