Simba yajipanga kuhuisha mikataba nyota nane

Ligi Kuu ya Tanzania Bara inamalizika mwezi ujao na tayari michakato ya usajili wa wachezaji imeanza kushika kasi

Nyota nane wa kikosi cha Simba mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu ambapo Mwenyekiti wa Simba Swedy Mkwabi amesema wako mbioni kuanza mazungumzo ya kuhuisha mikataba ya wachezaji hao

Miongoni mwa nyota ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu ni pamoja na Emmanuel Okwi, John Bocco, Jonas Mkude, Aishi Manula, Erasto Nyoni, James Kotei, Asante Kwasi na Shomari Kapombe

“Tunasubiri ripoti ya Mwalimu Aussems ili tuanze michakato ya usajili. Lakini bila shaka, wachezaji wengi tutaendelea nao” amesema

“Hakuna mchezaji yeyote ambaye mkataba wake wa kuitumikia Simba utakuwa umemalizika na tumempa ruhusa ya kuondoka kwa maana ya kwenda kujiunga na timu nyingine wote tuna mipango nao na tunaimani watasaini mikata mipya ya kubaki hapa.

“Bodi bado haijazungumza na mchezaji yeyote, ambaye mkataba wake unamalizika kutokana na majukumu ya mechi za kimataifa ambazo tunacheza mfululizo, lakini nadhani tutakaa nao na mambo yatakwenda sawa kwa pande zote mbili tutakubaliana”