
Licha ya kupoteza mchezo huo, Serengeti Boyz ilicheza vizuri na hakika hawapaswi kulaumiwa
Edmund John aliifungia Serengeti Boyz mabao mawili moja likiwa la mkwaju wa penati huku mengine mawili yakifungwa na Kelvin John ‘Mbappe’ na Morice Abraham (p)
Vijana wa Nigeria walifunga mabao yao kupitia kwa Olatomi, Ubani aliyefunga mabao mawili, Amoo na Abraheem
Mchezo unaofuata wa Serengeti Boyz ni April 17 dhidi ya Angola kabla ya kumaliza hatua ya makundi kwa kuchuana na Uganda April 20