Serengeti Boyz yapoteza mchezo wa kwanza AFCON U17

Timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 Serengeti Boyz, imeanza vibaya michuano ya AFCON U17 inyofanyika nchini baada ya kukubali kipigo cha mabao 5-4 kutoka kwa Nigeria katika mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa

Licha ya kupoteza mchezo huo, Serengeti Boyz ilicheza vizuri na hakika hawapaswi kulaumiwa

Edmund John aliifungia Serengeti Boyz mabao mawili moja likiwa la mkwaju wa penati huku mengine mawili yakifungwa na Kelvin John ‘Mbappe’ na Morice Abraham (p)

Vijana wa Nigeria walifunga mabao yao kupitia kwa Olatomi, Ubani aliyefunga mabao mawili, Amoo na Abraheem

Mchezo unaofuata wa Serengeti Boyz ni April 17 dhidi ya Angola kabla ya kumaliza hatua ya makundi kwa kuchuana na Uganda April 20