
Kagera Sugar ilikuwa bora zaidi kwenye kipindi cha kwanza ambapo ilipachika mabao yake mawili yaliyofungwa na Kassim Khamis na Ramadhani Kapera
Simba ilikuja juu kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kufunga bao lake kupitia kwa Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 64
Wekundu wa Msimbazi walikosa nafasi kadhaa ambazo zingewawezesha kuondoka na angalau alama moja dhidi ya Kagera Sugar ambayo kwa mara nyingine imedhihirisha umwamba wake dhidi ya Simba
Simba haikuwa katika kiwango bora leo, pengine uchovu uliosababishwa na timu kucheza mfululizo umechangia kukosa matokeo muhimu
Baada ya mchezo huo Simba inaelekea mkoani Mwanza ambapo Jumanne, April 23 itacheza na Alliance Fc