Simba yaelekea Mwanza

Baada ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar, kikosi cha Simba kimeondoka leo Jumapili asubuhi mkoani Kagera kuelekea Mwanza tayari kwa michezo miwili ya viporo itakayopigwa jijini humo

Keshokutwa April 23 Simba itashuka uwanja wa CCM Kirumba kuchuana na Alliance Fc na siku mbili baadae, April 25 Simba itarejea kwenye uwanja huo kuchuana na KMC kisha kikosi cha mabingwa hao watetezi kitaelekea mkoani Mara kuikabili Biashara United April 28