Heri ya sikukuu ya Pasaka kwa Wanamsimbazi

Wakristo nchini, leo wanaungana na wenzao duniani kusherehekea Sikukuu ya Pasaka ya kukumbuka ufufuko wa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2,000 iliyopita.

Maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na ibada kwenye makanisa mbalimbali nchini pamoja na burudani zitakazofanyika kumbi tofauti za starehe, fukwe za bahari na sehemu nyingine.

Sherehe hii ambayo kwa Wakristo huwakumbusha upendo, inatakiwa kusherehekewa katika hali ya amani na utulivu.

Tunawatakia Wanamsimbazi na Watanzania wote Pasaka Njema.