
Maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na ibada kwenye makanisa mbalimbali nchini pamoja na burudani zitakazofanyika kumbi tofauti za starehe, fukwe za bahari na sehemu nyingine.
Sherehe hii ambayo kwa Wakristo huwakumbusha upendo, inatakiwa kusherehekewa katika hali ya amani na utulivu.
Tunawatakia Wanamsimbazi na Watanzania wote Pasaka Njema.