Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amemtaka Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara kutofuatilia mambo yasiyomhusu.
Kauli ya Zahera imekuja kufuatia Manara kumsema kocha huyo kuwa amekuwa akiishutumu bodi ya ligi na TFF kuwa inafanya mpango wa kuiwezesha Simba kuchukua ubingwa wa ligi.
Ameeleza kwa kumtaka Manara ni vema akafuatilia mambo yanayomhusu na kuachana na kumzunguzia yeye kwani anaona anachokifanya ni sahihi.
Zahera amesema kamwe hatoweza kukaa kimya kwani kila anachokisema ni sahihi kwake na hataweza kufumbia macho madudu ya TFF.
Amefunguka kwa kusema kama TFF wanaona anakiuka taratibu wamfungie lakini hatoacha kuzungumza mpaka pale uongozi wa Shirikisho hilo utakapobadilika.