
Baada ya juzi kuichapa Alliance Fc mabao 2-0 kwenye uwanja huo, leo Simba inarejea tena ikiwa na shauku ya kuondoka na alama zote tatu
Kocha Mkuu wa mabingwa hao watetezi Patrick Aussems amesema wanatarajia kupata upinzani mkali kutoka kwa KMC lakini wamejipanga kupata matokeo yatakayowapandisha hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi
Ushindi utaiwezesha Simba kufikisha alama 66 na kuiondoa Azam Fc katika nafasi ya pili kutokana na wingi wa mabao ya kufunga
Katika mchezo wa duru ya kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa, Simba ilifanikiwa kuondoka na alama zote tatu kwa ushindi wa mabao 2-1 huku ikifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake
Leo pia Aussems amesema atafanya mabadiliko ya kikosi kwani mchezo wa leo unahitaji uzoefu na ufundi